Sekondari Mkoani Singida ; Zapatiwa Msaada Za Darubini...


 Daudi Jairo(kushoto), akimkabidhi darubini ofisa elimu Mkoa Singida Yusufu Kipengere, kwa ajili ya shule sekondari Mwenge.
Na:  Elisante John
KAMPUNI ya uuzaji vitabu G.B.S Ltd, ya Dar es Salaam, imetoa msaada wa darubini tatu zenye thamani ya Sh.825,000 Mkoani Singida kwa ajili ya shule ya tatu za Sekondari.
Shule zilizonufaika na msaada huo ni Mwenge (Iliyopo Manispaa Singida), Lulumba na Gumanga (Iramba.
Msaada huo umekabidhiwa na Meneja Kampuni ya G.B.S.Ltd kupitia ofisi zake zilizopo kanda ya kati(Dodoma), Daudi Jairo.
Jairo amesema, licha msaada huo kuwa na lengo la kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi, pia ni kuhakikisha mwanafunzi wa kwanza nchini anatokea Mkoa Singida.
Alisema kuanzia mwaka 2009 hadi sasa kampuni hiyo imetoa msaada wa vifaa mbali mbali vya kujifunzia shule za Sekondari, wenye thamani zaidi ya Sh.Milioni tisa Mkoani Singida.
Kila darubini iliyotolewa msaada ina thamani ya Sh. 275,000.
Akipokea darubini hizo kabla ya kukabidhi kwa walengwa, afisa elimu Mkoa Singida Yusufu Kipengere alisema kuwa, Mkoa huo una jumla ya Sekondari 153, lakini ni shule saba tu ndizo zenye maabara za kufanyia mtihani. 

Aidha kupitia msaada huo, aliwaagiza wakuu wa shule zilizonufaika na darubini hizo kutokuwa wachoyo kwa shule zitakazoomba kuzimwa, kwa ajili ya wanafunzi wa shule jirani kujifunzia.