"MAFANIKIO NILIYONAYO HAYATEGEMEI MKONO WA MWANAUME".......ODAMA


Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka na kuweka wazi  kuwa katika mafanikio aliyoyapata hakuna mkono wa mwanaume kama ilivyo kwa wasichana wengine mastaa wa mjini.Odama ameeleza  kuwa amekuwa akifanya kazi kwa bidii na kile anachokipata ndicho anachofanyia mambo yote ya maendeleo ambapo hadi unaposoma hapa, anamiliki kampuni yake ya filamu ya J-Film For Life, magari mawili na mjengo.

“Mafanikio yangu yametokana na kazi zangu mwenyewe na hakuna mkono wa mwanaume, sitaki iwe hivyo ‘coz’ ndiyo maisha niliyoyachagua ya kutomtegemea mtu kwani kile ninachokipata kwenye filamu zangu ndicho kinachonipa maendeleo haya,” alisema Odama.

Hata hivyo, mwanadashosti huyo alisema kwa sasa ana mchumba na anatarajia kufunga ndoa mwakani.