Askari
 wa Jeshi la Polisi wakijihami na matambara pamoja na mifuko ya nailoni 
ili kumdhibiti mtuhumiwa aliyejipaka kinyesi mwili mzima na kutaka 
kuwakimbia askari kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es 
Salaam. Mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja 
alidaiwa kuwa ni mwizi wa simu lakini hakimu alimwachilia huru kutokana 
na kukosekana ushahidi hata hivyo askari waliendelea kumshikilia tena 
jambo ambalo lili muudhi na aliporudi mahabusu aliamua kujipaka kinyesi 
mwilini.
Askari wakimdhibiti mtuhumiwa huyo kwa kutumia matambara na mashuka mazito kutokana na kuwa na kinyesi kingi.
Akipandishwa kwenye gari la polisi na kuondoka nae.
Akilazimishwa kuvaa nguo.
Akiondolewa eneo hilo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
 
