BHOKE WA BBA ATEULIWA KUWA BALOZIA TAASISI YA KUPAMBANA NA FUNZA WA MIGUU

Aliyewahi kuwa mwakilishi wa Tanzania katika shindano la Big Brother Africa, 2011, Bhoke Egina ameteuliwa kuwa balozi mpya wa Tanzania wa taasisi ya Ahadi Trust Tanzania. Bhoke alikuwa akisherehea siku yake ya kuzaliwa weekend iliyopita na kuitumia pamoja na rafiki zake kutumia siku hiyo kampeni dhidi ya funza wa miguuni.
Mguu ulioathiriwa na funza
Tukio hilo lilifanyika mjini Moshi ambapo mwenyekiti mtendaji wa Ahadi Kenya , Stanley Kamau alimtangaza Bhoke kama balozi wa Tanzania na kuonesha kufurahishwa kwake na mastaa wanaoguswa na kuhudumia jamii hasa katika mapambano dhidi ya funza ambao ni tatizo barani Afrika.

Hafla hiyo ilihudhuria pia na mshindi wa BBA mwaka 2007, Richard Bezuidenhout.Bhoke alikuwa ni miongoni wa washiriki wa mwaka 2011 wa BBA walioenda Thika nchini Kenya kuwasaidia watoto walioathiriwa na funza ambapo anasema hakulijua tatizo hilo mpaka alipowaona watoto hao.