Clement Mbawala; CHADEMA Wajichanganya Uingereza!


Chama Cha Demokrasia na Maendeleo jana kiliendelea kulalamikiwa na Watanzania kwa kukosa DIRA ya uongozi hasa baada ya kujichanganya,kubishana wenyewe kuhusu msimamo wa SERA yao hapa UK. Haya yaliwakuta katika kikao cha kutafuta wanachama kilichofanyika jana tarehe 27/08/2012 katika Mji wa Reading, UK.
Watanzania wachache waliohudhuria mkutano huo walinung'unika kuwa kikao hakikuwa na utaratibu na mtirirko wowote wa uendeshaji wa vikao na ulibagua uchangiaji wa kijinsia na ulijali zaidi ukabila.
 
Akilalamika huku akitoka nje ya ukumbi ndugu aliyejitambulisha kuitwa Said alisema kuwa Kikao hiki kiliandaliwa kwanza na Wachaga tu waliochangishana fedha na hivyo wakati wa kikao hawakutoa nafasi huru kwa watanzania wengi kushiriki kikamilifu zaidi ya kuambiwa watoe fedha kuchangia Chama na mfuko wa kuzikana.
Mwingine ni Bi Rehema aliyesema kuwa ameshangazwa na kauli ya Bw. Prudence aliyesema kuwa yeye ndiye ameachiwa jukumu la kueneza Sera na Siasa za CHADEMA na hivyo ni lazima achangishiwe fedha za kuzunguka UK ili aandae akina mama wasomi wajiunge Chadema ili wapewe nafasi za Ubunge wa Viti Maalum katika uchaguzi mpya 2015 maana wengi wa waliopo muda wao umekwisha na kuwa Viongozi wa Chadema wanajali kundi la akina mama. 
 
Nanukuu..''eti anatuambia mambo ya viongozi kujali wanawake na siyo Sera ya Chadema juu ya wanawake...yeye mwenyewe ametelekeza mke na watoto wake bongo..wanaomba omba tu huko yeye anakula raha na bado anataka michango yetu zaidi....jana tu alikuwa ndiyo kada mwandamizi wa CCM hapa UK akatengwa kwa sababu ya tabia zake...sisi siyo wajinga bwana..''
Ramadhani aliongea kwa mfadhaiko akishangaa kuwa Dkta Jona LUSINGU ni Wakala wa Chadema huku alikuwa ni Kiongozi wa Jumuiya ya Tanzania UK aliyeshindwa kazi na kukimbia uongozi mwenyewe bila kukabidhi ofisi na sasa atawezaje kusimamia siasa za Chadema ..''au ndiyo kuyeyushana tu..''. Alihamaki akiwa anatoka mlangoni na kuunyosha mkono kuelekea kwa Dk Lusingu aliyekuwa amekataliwa nafasi ya kukaa meza ya viongozi na hivyo kukaa na washabaki wachache waliokuwepo.
 
Alipopewa nafasi ya kuongea Dkt Lusingu alizidi kuwachanganya viongozi na mashabiki wachache waliohudhuria pale aliposema ''Chadema imekuwa haina sera ya Diaspora na Mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa na Chadema kuingia madarakani Tanzania na hasa uongozi wao wa kitaifa uliopo sasa isipokuwa pale ambapo mfumo mzima wa utawala utakapobadilika na chadema kuwa chama cha kitaifa kuliko hivi sasa''. 
 
Aliongeza kwamba matawi ya nje ya Chadema yanaweza yasiwe na manufaa iwapo kama yatatelekezwa kama walivyofanya CCM.Aliongeza kuwa ni kweli toka Chadema imekuja hapa UK kumekuwepo na manung'uniko miongoni mwa Watanzania na ni vema kujipanga upya na uongozi msafi. Dkta Lusingu aliyekatishwa kuongea alikuwa ni mmoja wa viongozi wa awali wa shina la CCM Reading
MwanaCCM mmoja anayeitwa Chris alidokeza kuwa waliohudhuria mkutano huu sehemu kubwa ni wanaCCM walioingia kusikiliza kipya gani watani wamefuatia nazo nyayo lakini wameona hakuna jipya bali maumivu ya kukosa SERA. 
 
Alisema kuwa CCM UK imekuwa na mapendekezo mengi katika vikao vya Taifa na serikali imeanza kushughuliia kero nyingi za wanaDiaspora ikijumuisha kumalizia mpango mahsusi wa kueneza na kuleta UK huduma za kifedha na hifadhi za jamii kuliko danganya toto ya Chadema ya kuchangia mfuko wa mazishi..
 
''yaani chadema wanaona umuhimu wa Mtanzania pale anapokufa tu na wao kumzika..'' Alidokeza kuwa ni uonevu kumtwisha mdogo wake Dkta Lusingu mzigo wa Chadema wa kuchangia vifo.. ''Wakati Jeladi Lusingu alipofiwa na mkewe ni wanaCCM waliongoza kuhimiza kufa na kupona miji yote ya UK ili kusaidia safari na hifadhi ya mwisho ya mama huyo. Leo sera za umoja zilizomsaidia anazipinga au amelazimishwa tu?''
 
Baada ya kikao kuisha Bw. Prudence alitamba kwa wenzake kuwa alipokuwa CCM UK kila mkutano walikuwa wakichangishana ili kuhudumia kikao na usafiri na sasa wanachama wamechoka kifedha na hivyo sasa Chadema imeanza kumwaga pesa kuwamaliza CCM kabisa hapa UK. Prudence alipoombwa mahojiano ya ana kwa ana alisema hana muda.
 
Mwandishi alitafuta na kupatiwa namba ya simu ya Mwenyekiti wa CCM UK ili kupata mawazo yake juu ya mkutano huu wa Chadema hapa Reading lakini alisema yupo Edmonton, London kuhudhuria CCM UK 
 
BBQ-Outreach Party iliyoandaliwa na wanaCCM North London tangu miezi miwili iliyopita hivyo asingeweza kuahirisha lakini anayo nafasi ya mahojiano baada ya siku hiyo. Pia alisema CCM ilikaribisha upinzani Tanzania na inaendelea kuikaribisha Chadema hapa UK.
 
Na Mwandishi wa kujitegemea,
Clement Mbawala.
Tanzania Now.
Slough.Berkshire.