Producer J-Ryder Ameikosoa Nyimbo Mpya ya Professor Jay Feat Dully-Hello

Katika uchambuzi wa wimbo mpya wa professor Jay uliofanywa na blog ya leointerment producer J Ryder ametoa uchambuzi wake wa wimbo huo mpya kama ifuatavyo:"Autotune effect kwenye verse ya kwanza haijakaa poa, ukiimba off key sio rahisi ikubali siku zote...
Beat iko okay, ila kuna vitu kibao vya kurekebishwa...afu inaonekana kama imefanywa tu usiku fasta fasta, asubuhi ikaachiwa...haha labda...na hizi haraka za fiesta.
Pia ni kwamba inafanana na beats zingine alizowahi tengeneza...

Kingine ukisikiliza kwa makini sana..unaona sound ina compression/ limiter zaidi ama quality sio nzuri..

Na upande wa quality, sounds alizotumia mfano ikiwa ni Vst's, then iyo vst instrument yenyewe haikua recorded/ sampled properly...ndio maana sounds zinatofautiana, na pia ndio maana professional sound quality vst's cost thousands...simply 'cuz the technology used on the recorded instruments is up-to-date vinginevyo beats nyingi zina sound sawa kama they use kitu kile kile..


Chorus Dully alivyoimba nimeipenda...safi sana, background vocals za Dully kwenye verse za prof j sio kivile...na zingine zipo off key..

And most beats, unakuta wanapenda kutumia 'swing' fulani..ni freshii na inaleta groove..but naona inatumiwa sana hadi flavour yake ina fade away..

Vinginevyo, Prof. J ali-deserve beat kali zaidi ya hii, kwasababu ni msanii mkubwa na wa muda mrefu kwenye hii Music Industry ya Tanzania." Says J Ryder