UFAHARI WA MAGARI YA KUKODI WAMPONZA JACK WA CHUZ


MWIGIZAJI wa Kibongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kukodi gari aina ya Totota Spacio lenye namba za usajili T 750 BPK na kushindwa kulipa.
jicholetu iliambiwa na aliyemkodishia kuwa Jack Chuz alipewa gari hilo alitumie kwa siku tano kwa makubaliano ya kulipa elfu 50 kwa siku lakini zilipomalizika, alilirudisha na nusu ya fedha hivyo anasakwa na polisi kwa jalada la kesi namba RB/CH/ 6031/2012