RONALDO AZITAMANISHA MAN UNITED NA CITY.
MSHAMBULIAJI nyota wa
kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameziweka
klabu za Manchester United na City kujiweka tayari kumsajili baada ya
kukiri kuwa anataka kuondoka Madrid. Chanzo
kimoja cha habari nchini Hispania kilihabarisha kuwa nyota huyo
alimwambia rais wa Madrid kuwa anataka kuondoka kwa kile kilichodaiwa
kushindwa kuelewana na baadhi ya wachezaji wenzake. Hali
hiyo ya kutokuwa na furaha kwa Ronaldo mwenye umri wa miaka 27
ilionekana wazi wakati wa mchezo wa Jumapili baina ya Madrid na Granada
ambapo alishinda mabao mawili lakini hakushangilia. Akihojiwa
kuhusiana na tukio hilo nyota huyo amesema kuwa alikuwa katika majonzi
na viongozi wa klabu hiyo wanajua sababu hivyo hawezi kusema zaidi
kuhusiana na hilo. Kauli
hiyo inazitamanisha klabu za United, City pamoja na Chlesea kumsajili
mchezaji huyo ambapo hivi sasa watakuwa wakifuatilia mstakabali wa
mchezaji huyo katika klabu hiyo.