US OPEN: SERENA ATINGA ROBO FAINALI KWA KISHINDO.
MCHEZAJI nyota wa tenisi
kutoka Marekani, Serena Williams amefanikiwa kutinga robo fainali ya
michuano ya wazi ya Marekani baada ya kumsambaratisha Andrea Hlavackova
kwa 6-0 6-0. Serena
ambaye ni bingwa mara tatu wa michuano hiyo atapambana na Ana Ivanovic
aliyemfunga Tsvetana Pironkova kwa 6-0 6-4 katika mzunguko wa nne. Katika
mchezo wa wawili wawili Serena na dada yake Venus Williams walishindwa
kutamba mbele ya Maria Kirilenko na Nadia Petrova kutoka Urusi baada ya
kufungwa kwa seti 2-0 za 6-1 6-4. Kwa
upande wa wanaume Andy Murray wa Uingereza alifanikiwa kutinga katika
hatua ya robo fainali ya michuano hiyo baada ya kumfunga Milos Raonic
kwa 6-4 6-4 6-2.