VAN PERSIE MAJERUHI. 

 
MSHAMBULIAJI wa kimataifa
 wa Uholanzi na klabu ya Manchester United, Robin van Persie alitolewa 
nje katika kipindi cha mapumziko baada ya kupata majeruhi nyuma ya paja 
katika mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza michuano ya Kombe la Dunia 
2014 dhidi ya Hungary ambapo timu yake ilishinda mabao 4-1. Kocha
 wa Uholanzi Louis van Gaaal amesema kuwa alimbadilisha mchezaji huyo 
kwa tahadhari ili asiumie zaidi kwenye mchezo huo ambao mpaka mapumziko 
walikuwa wakiongoza kwa mabao 2-1. Mabao ya timu hiyo kwenye mchezo huo 
yalifungwa na Jeremain Lens aliyefunga bao la kuongoza kabla ya Balazs 
Dzsudzsak wa Hungary kusawazisha kwa penati lakini Martin Bruno Indi 
aliongoza bao la pili na kupelekea timu hiyo kwenda mapumziko ikiwa 
inaongoza. Mabao mengine ya Uholanzi yalifungwa na Lens ambaye alifunga 
mabao mawili katika mchezo huo na Klaas-Jan Hunterlaar aliyepigilia 
msumari wa mwisho kwenye jeneza la Hungary na kuihakikishia Uholanzi 
kuondoka na lama zote tatu. Baadhi ya michezo mingine iliyochezwa jana, 
Hispania ilifanikiwa kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya 
Georgia huku Ufaransa wakiibugiza Belarus kwa mabao 3-1 wakati Ujerumani
 nao wakiendeleza wimbi la ushindi kwa kuisambaratisha Austria mabao 
2-1.