Maaskari wakiwa kwenye ulinzi wakati wa maanadamano ya wanachuo waliokuwa wanaelekekea kwa mkuu wa mkoa Dodoma
Uvumilivu sasa umetushinda!!! Hizi ni kauli za wanafunzi wengi wa chuo Kikuu cha St.John walivyosikika wakizungumza kufuatia kile ambacho kimeendelea kuvikumba baadhi ya vyuo hapa nchini.
Usiku wa kuamkia leo baadhi ya wanachuo walivamiwa chumbani na baadhi ya watu wasiofahamika ambao walikata nondo za dirisha na kuiba Laptop tatu na simu tano na baada ya kuchukua vitu hivyo waliacha wamewafanyia vitendo vibaya na pia wanafunzi hao waliachwa wamefungwa ili wasipige kelele.
Usiku wa kuamkia leo baadhi ya wanachuo walivamiwa chumbani na baadhi ya watu wasiofahamika ambao walikata nondo za dirisha na kuiba Laptop tatu na simu tano na baada ya kuchukua vitu hivyo waliacha wamewafanyia vitendo vibaya na pia wanafunzi hao waliachwa wamefungwa ili wasipige kelele.
Hali imepelekea hisia kali za wanafunzi wa chuo hicho na kuamua kufanya maandamano kupinga vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na haki za kibinadamu na kusababisha hali ya wanafunzi hao kusoma kwa mashaka kutokana na mwendelezo wa matukio hayo.
Wanafunzi hao waliandamana leo kuelekea katika ofisi za mkuu wa mkoa, kwa madai ya kutaka kukutana na mkuu huyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi ya mkoa pamoja na kuhitaji kukutana na RPC kama katibu wa kamati ya ulinzi ya mkoa ili wafikishe vilio zaidi.
Hata hivyo walisimama na kukaa kwa muda katika viwanja vya Nyerere square walipokuwa wakimsubiri mkuu wa mkoa. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari mkuu huyo wa mkoa hakuweza kuja katika viwanja hivyo, hatua iliyowalazimu wanafunzi hao kurudi chuoni.
Wanachuo wakiwa wameshika mabango ya kushinikiza ulinzi katika chuo cha St. John
Wanachuo wa chuo kikuu wakiwa kwenye maandamano
Maaskari wakiwa nyuma ya maanadamano ya wanachuo wa chuo kikuu cha St. John
Wanachuo wakiwa kwenye maandamano kuelekea kwa mkuu wa mkoa hii ni kushinikiza ulinzi kwa sababu ya matukio ambayo yanaendelea kutokea maana juzi alifariki mwanachuo.