Vituko
 mjini Iringa haviwezi kuisha kama jamii haitakubali kwa moyo mmoja 
kupambana na ukatili wa kijinsia. Huyu ni Binti ZAWAD KARIM miaka 16 
mkazi wa mshindo nyuma ya banki ya NBC manispaa ya Iringa amepigwa na 
hatimaye kunyweshwa mkojo na mama yake mdogo aitwaye Ever ubamba.
Tukio lilikuwa hivi:
Zawadi  kimsingi anaishi na mama yake mzazi ambaye kwa kipindi 
hicho dada mtu huyo alikuwa anaumwa. Ever alikuwa nje na marafiki zake 
ndipo mama yake mdogo huyo akamwiita ndani ya nyumba yao hiyo wanayoishi
 mtaa wa mshindo.
Baada ya kumwita na kisha mtoto huyo kushindwa kusikia baadaye 
aliitika na kuingia ndani na  ndipo alipo ambiwa avue nguo zote na huyo mama yake  mdogo Ever .Baada ya muda mfupi Zawadi 
alianza kupokea kipigo kikali kutoka kwa mama yake  mdogo.
Katika kipigo hicho Zawadi  alipigwa pamoja na 
kunyweshwa mkojo kutoka kwa mama yake mdogo huyo.Zawadi ambaye ni mtoto 
wa kuzaliwa na Dada yake Ever inadaiwa kipigo hicho kimesababishwa na 
tuhuma kwamba eti familia hiyo haina mtoto kama yeye zawadi.
Zawadi inadaiwa aliwahi kwenda zanzibar kwa nia ya kufanya kazi na 
baada ya muda mama yake mzazi ambaye jina lake bado halijafahamika 
alimpigia simu arudi nyumbani na mara baada ya kurudi ndipo 
kutokuelewana huko kukajitokeza.
Aidha taarifa za ndani kuhusu tukio hilo zinasema kuwa Mama yake 
Msichana Zawadi alitupwa akiwa mchanga na kuokotwa na wasamalia wema na 
hatimaye kulelewa na Bibi yake ambaye hata hivyo amefariki duni.
Kisa cha yote hayo ni madai ya mtoto zawadi kuomba aoneshwe Baba yake 
mzazi ili walau aweze kupata pumziko la adha anazo zipata kutoka kwa 
ushirika wa ndugu zake hao.Zawadi pamoja na majirani wameuambia mtandao 
huu kuwa vitu vilivyo tumika kumwadhibu vilikuwa ni pamoja na nyaya za 
simu,mkandaa,na vipande vya chupa katika kumchoma navyo.
Hata hivyo hadi mtandao huu unachapisha taarifa hii watuhumiwa wa 
tukio hili yaani Mama mzazi pamoja na Mama mdogo wa Zawadi wanashikiliwa
 na jeshi la polisi kitengo cha dawati la jinsia kwa mahojiano zaidi.
Chanzo: francisgodwin
