Baada ya Diamond, Diva kumshirikisha Kabayser na Ommy Dimpoz


Baada ya mtangazaji wa radio na msanii wa muziki Loveness aka Diva kuachia wimbo ‘Piga Simu’ aliomshirikisha Diamond, safari yake ya muziki haina dalili ya kusimama hivi karibuni kwakuwa ana mipango mikubwa na kufanya ngoma na ‘big cats’ in the game.

“Whatchu all think? Remix coming featuring Ommy Dimpoz na ndio video tutatoa sasa with the boys,Ommy Dimpoz and Diamond …all we need is something good not only a video but Diva kinda video …next level kabisa, the moment ntarelease remix and the video will continue sasa,” aliandika kwenye blog yake.
“Second song itakuja featuring Mr. Blue na ntaitoa after Diva Giving for charity event and namtafuta Blue for that muda si mrefu sana. He is the perfect feature for my second song, ana fit as in my verses are ready and the beat omg Fishcrab again as u know.”
Katika hatua nyingine baada ya kuongezeka kwa maswali mengi juu ya nani aliyemwimbia kwenye ‘Piga Simu’ mwezi uliopita na kuandikwa vibaya aliamua kufunguka na kutoa ufafanuzi.
‘Sijataja mtu jina …and are you sure huyo unaemuhisi au unayemtaja natoka nae? maana nilivyosema sina boyfriend for years mlisema Diva msagaji Diva this Diva that , nasema nina boyfriend nimemuimbia nyimbo mnaanza sasa kunitajia list ndefu , you guys got time I swear,you all don’t know a bit about me,” aliandika.
“Acheni kuzusha mambo ya ajabu na kusambaza,maana asilimia ya mambo ninayoandikwa na kuongelewa that’s so not me , nijueni basi kidogo ndo mnizungumzie.”


Aliendelea kuandika, “Tupeane break sasa, mjueni Mungu a bit maana it’s too much sasa. Next thing what???Diva freemason labda maana ndio zenu hizi mpya while am a very Good Christian and church is the right thing for me every sundays . Serious what next jamani??? What next?? Da! maana nimechoka sana sana.”