BUNGEN: MHESHIMIWA MANYANYA AITUHUMU CHADEMA KUMDHURU DOKTA ULIMBOKA!!


Katika hali ya kustaajabisha wakati nikiwa naangalia Bunge leo jioni muda wa saa moja nilishangaa kumuona Injinia na Mbunge wa viti maalumu mkoani Ruvuma Bi. Stella Manyanya akichangia hoja inayohusiana na Dokta ulimboka ambapo alitamka wazi kuwa watu waliomteka Dokta huyo walikuwa wamevalia magwanda hivyo bila ya kukosea hao watu watakuwa ni wanachama wa chama cha Chadema kutokana na mavazi yao licha ya kuwa
Dokta mwenyewe alisikika akiwataja baadhi ya muonekano wa watu waliomteka kwa mujibu wa vyombo vya habari na hata Mh. Mnyika alipokuwa akimjibu Mbunge huyo kwa kunukuu kauli ya Dokta, sasa hapa tuamini upande upi na nani anaongea ukweli