Balotelli kupima ili kujua kama ni baba wa mtoto wa Raffaella



Mshambuliaji wa Manchester City na timu ya taifa ya Italia Mario Balotelli juzi ameviambia vyombo vya habari nchini Italia kuwa atachukua vipimo (paternity test) vya hospitali ili kujua kama yeye ndo baba wa mtoto ambaye mpenzi wake wa zamani anadai kuwa na ujauzito naye.

Raffaella Fico, 24, nyota wa TV na model wa nguo za ndani, aliliambia gazeti la kila wiki la Chi kuwa anategemea kupata mtoto wa Balotelli.
“Nikithibitisha kuwa mimi ndo baba, ntachukua majukumu yote,” alisema Balotelli mwenye miaka 21, kwenye maelezo yake.
“Nilifahamu kupitia kwa mtu mwingine siku chache zilizopita kuwa Raffaella ni mjamzito. Ndio maana niliamua kuwasiliana naye na hapo ndipo aliponiambia kuwa ni kweli.”
“Nimejisikia vibaya, sidhani kama ni kawaida kutoelezwa chochote mpaka mwezi wanne wa ujauzito.”
Uhusiano wa miezi 18 wa wapenzi hao ulikuwa ukizungumzwa na kuandikwa mara kwa mara kwenye vyombo vya habari vya Italia kabla hawajaachana mwezi April mwaka huu.