SHIGONGO AKANUSHA KUMUOMBA RADHI JOSE CHAMELEONE


 
Hii ni picha na maneno ya kuomba radhi yanayodaiwa kutolewa na Eric Shigongo ambayo yamewekwa kwenye mtandao wa Uganda, ikiwa ni propaganda za kitoto za Chameleone za kujaribu kujikosha kwa mashabiki zake. 
Awali, picha na maneno haya yaliandikwa kwa Kiswahili kibovu na kuwekwa kwenye Fan Page ya Chameleone kwenye facebook, alipoona watu wameshitukia Kiswahili kibovu kilichotumika ambacho hakiwezi kuwa cha Shigongo, wakaamua kuondoa pamoja na taarifa zingine za kipuuzi alizokwisha weka. 

Hivi sasa picha hii imebadilishwa na kuandikwa kwa Kiingereza cha Kiganda na kisha kuwekwa kwenye mtandao wa Uganda, mtaona ni kiasi gani zinafanyika kampeni za kutaka kumsafisha Chameleone ambaye alishachafuka siku nyingi! Shigongo HAS NEVER, AND HE NEVER APOLOGISE TO 'Dr. Jose Chameleone'!