Wema Sepetu na Diva waunga List ya kusaidia wasiojiweza


Wema-Sepetu
Muigizaji wa filamu nchini na Miss Tanzania wa zamani (2006),Wema Sepetu anatarajiwa kwenda jijini Arusha mwezi huu na kushiriki uoashaji wa magari ili kukusanya fedha za kusaidia watu wasiojiweza jijini humo.

“On 14th July I will be in Arusha with manager kushiriki uoshaji wa magari ili kuchangia fedha za kusaidia wasiojiweza in Arusha,” alitweet jana.
Mwingine aliyeamua kujitolea nguvu na mali kuchangisha fedha kwaajili ya kuwasaidia watoto yatima ni mtangazaji wa Clouds Fm, Loveness aka Diva.

Kupitia website yake, Diva amesema, “So nimeamua kwa muda mrefu sana kutoa for charity and right now am too busy organizing this charity event inayoitwa Diva giving for charity. Aim is raising much needed funds to support orphans.
June na July imekuwa miezi iliyotumiwa zaidi na mastaa wa hapa nchini kusaidia vituo vya watoto yatima.
June 30, mwanamuziki Lady Jaydee pamoja na familia yake walikitembelea kituo cha watoto yatima cha Maunga Centre kilichopo Kinondoni jijini Dar es Salaam na kutoa misaada mbalimbali ikiwa pamoja na kushiriki chakula cha mchana na watoto hao.
Katika hotuba yake, kituo hicho kilisema kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na kukosa fedha za kuwalipa wahudumu, Kukosa eneo kubwa la kujenga kituo, Kukosa wafadhili, watoto kutokuwa na sare za shule na kukosa gharama za kuwasomesha (michango ya shule).
Lady Jaydee aliwaahidi kuwatafutia kiwanja kikubwa kwaajili ya kujenga kituo kingine na kusema kuwa iwapo akitokea mtu wa kuwasaidia kiwanja, watachangisha fedha za kuanza ujenzi huo.
Naye muigizaji wa filamu mwenye mafanikio makubwa nchini Raymond Kigosi aka Ray The Greatest, weekend iliyopita alikitembelea kituo hicho cha Maungo na kutoa msaada sambamba na uzinduzi wa filamu yake mpya ya Sobbing Sound.
Kupitia blog yake Ray alisema: “Hili ni jukumu la watanzania wote kuanza kuguswa katika hili maana hapa duniani sisi ni wapangaji tu makazi yetu ni kwa Mungu Baba, sasa unapopata kidogo jaribu kuwafikiria na wale waliokuwa na maisha magumu, yaani tugawane umasikini.”