Bahanuzi arejea kupata ubani kijijini



DORIS MALIYAGA
DUME la mabao la Yanga, Said Bahanuzi anatarajia kutua leo Jumamosi jijini Dar es Salaam akitokea kwao Mwanza alikokwenda kusaka baraka baada ya kupapotea kwa miaka mingi. Bahanuzi, ambaye nyota yake imeng'ara baada ya kutua kukitumikia kikosi cha Jangwani chini ya kocha Tom Saintfiet kwenye michuano ya Kombe la Kagame akitokea Mtibwa Sugar.

Ameliambia Mwanaspoti kuwa:"Nimeamua kufanya hivyo kwa sababu ni kipindi kirefu, niliasi nyumbani, nikaona nifanye hivyo baada ya kupata nafasi hii kwetu ni Sengerema, Mwanza."

Akizungumzia furaha yake baada ya kukamilisha ndoto zake za kuitwa Taifa Stars, Bahanuzi alisema: "Nilitamani kwa kipindi kirefu kucheza Taifa Stars hatimaye ndoto zangu zimefanikiwa. Nataka k