FINA MANGO KUMHOJI RUGE MUTAHABA KWENYE KIPINDI CHA MAKUTANO SHOW LEO JUMAMOSI

Wiki hii kwenye kipindi kipya cha radio cha Makutano Show kinachorushwa kila siku za Jumamosi kupitia Magic FM, mmoja wa mabosi wa Clouds FM Ruge Mutahaba atahojiwa na mtangazaji wa show hiyo Fina Mango.
Kwa namna yoyote interview hiyo itavuta wasikilizaji wengi hasa kwakuwa Fina atakuwa akimhoji bosi wake wa zamani  kipindi anafanya kazi Clouds FM.

Licha ya Fina Mango kuachishwa kazi pamoja na Masoud Kipanya, bado ameendelea kuwa karibu na Ruge ambao wanamiliki pamoja kampuni ya One Plus Communication.

Bila shaka itakuwa interview ya kuvutia.