SHUJAA WA OLIMPIKI MO FARAH ASONONESHWA KUONDOKA RVP ARSENAL.
MWANARIADHA shujaa wa
mbio za Olimpiki zilizofanyika jijini London ambaye ni shabiki wa
kutupwa wa klabu ya Arsenal Mo Farah ameeleza masikitiko yake baada ya
mshambuliaji nyota wa klabu hiyo Robin van Persie kuhamia Manchester
United. Farah
mwenye miaka 29 ambaye ni mshindi wa medali mbili za dhahabu za olimpiki
katika mbio za mita 10,000 na 5,000 amesema kuwa pamoja na kusikitishwa
kuondoka kwa mchezaji huyo lakini amemuelewa kwa uamuzi wake akiwa kama
mwanamichezo. Mwanariadha
huyo raia wa Uingereza mwenye asili ya Somalia aliendelea kusema Van
Persie anahitaji mataji ndio maana ameamua kuhama na hilo ni jambo la
kwawaida katika mchezo wa soka tofauti ilivyo katika riadha na anadhani
aliona ni vigumu kupata mafanikio hayo akiwa katika klabu hiyo. Farah amesema akiongea kama mshabiki amehuzunishwa sana Arsenal kumkosa mchezaji wa kiwango kama cha Van Persie.