"NDOA HAIWEZI KUNIFANYA NISIENDE CLUB"......KASHI


MWIGIZAJI wa filamu za Kibongo, Jaji Khamis ‘Kashi’ ameweka wazi kuwa pamoja na ndoa bado anafurahia maisha ya kuzama klabu kama kawa bila mumewe aliyetajwa kwa jina moja la Mussa.

Juzikati mpekuzi ilimnasa Kashi katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar akijiachia kwa raha zake ambapo alidai ndiyo kawaida yake kuzama viwanja tofauti bila kuambatana na ubavu wake.