BANZA: Niliwahi kulala na Otilia


NYOTA wa Bendi ya Extra Bongo, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ amefunguka kuwa amewahi kulala kitanda kimoja, shuka moja na mkatanyonga wa Extra Bongo, Otilia Boniface.
Akiling’ata sikio chanzo chetu cha habari, Banza alisema kila walipokuwa wakienda safari za mikoani, yeye na Otilia walikuwa wakimbonji pamoja lakini bila kukutana kimwili.
“Unajua mimi na Otilia tunafanya kazi hii ya muziki kwa kipindi kirefu katika bendi mbalimbali hivyo tumeshazoeana, hata tuliposafiri tulilala wote na sikuwahi kumuomba penzi,” alisema Banza.
Kwa upande wake, Otilia alipoulizwa kuhusu madai hayo ya Banza, alisema: “Ni kweli. Tena nilikuwa nampigia simu mchumba wangu na kumwambia niko na Banza kitandani, lakini hakushangaa.”