BREAKING NEWS: YANGA YAMSAJILI FRANK DOMAYO KWA MIL.20

Habari rasmi kutoka kwenye kamati ya usajili ya klabu ya Yanga ni kwamba timu hiyo leo imekamilisha usajili wa kinda la timu ya taifa ya Tanzania aliyeng'ara kwenye mchezo wa jumapili iliyopita dhidi ya Gambia Frank Domayo.
Domayo ambaye alikuwa akiichezea JKT Ruvu msimu uliopita, amesaini mkataba wa miaka 3 kuitumikia Yanga, huku akilipwa shilingi millioni 20 kama ada ya usajili na atakuwa akilipwa shilingi millioni moja kama msharaha kwa miaka 3 ijayo.