Redd's Miss Dar City Center 2012 ni Matilda Martin

 Redd's Miss Dar City Center 2012,Matilda Martin akipunga mkono muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi wa taji hilo usiku huu kwenye ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip,Jijini Dar es Salaam.

 Redd's Miss Dar City Center 2012,Matilda Martin (katikati) akiwa na mshindi wa pili wa taji hilo,Magdalena Munisi (kushoto) na Mshindi wa tatu,Witness Michael muda mfupi baada ya kutangazwa kwa washindi hawa katika shindano lililomalizika usiku huu kwenye ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip,Jijini Dar es Salaam.
 Washiriki waliotinga tano Bora ambao wote wanaenda moja kwa moja kujiunga na wenzao kwenye mashindano ya kanda ya Ilala,jijini Dar.
 Redd's Miss Dar City Center aliemaliza muda wake,Alexia William 
 Washiriki wote stejini.
 Tano Bora.
 Majaji wakijadiliana jambo kabla ya kumtangaza mshindi wa Redd's Miss Dar City Center 2012 usiku huu.
 Ankal Albert Makoye akitoa muongozo kwa Majaji.
 Redd's Miss Tanzania 2011/12,Salha Israel pia alikuwepo kushuhudia onyesho hili.
 Wadau wa Kamati ya Miss Tanzania.
 Diamond akiwa amenyanyuliwa juu juu na wacheza shoo wake.
 Shoo ya Diamond imekolea. 
Wema Sepetu akifuatilia Shoo ya Diamond usiku huu,huku tabasamu zito akilionyesha. 
 Diamond akipagawisha mashabiki wake.
 Mmoja wa Majaji wa Shindano hilo,Wema Sepetu akiuliza maswali kwa warembo walioingia tano bora.
 Mwanalibeneke wa Bongo Star Link,Hugo Martin a.k.a Dj Choka akiwajibika.
 Shamim Mwasha a.k.a Zeze a.k.a Mama IQ a.k.a Mama wa 8020 Fashions na a.k.a nyingi tu zingine akiwa kidigitali zaidi.....Utamtakaaaaaaaa.....
 Ben Kinyaiya,Bob Junior na rafikiye wakifatilia shindano hilo.
Meneja wa Kilaji cha Redd's Original,Victoria Kimaro (kushoto) akiwa na marafiki zake.
Mkuu wa Itifaki wa Kamati ya Miss Tanzania,Ankal Albert Makoye akiwakilisha kama kawa.
Idadi ya watu