GODZILLA : MASHABIKI WALITAKA NIIMBE

 

Staa wa hip hop Bongo, Godzilla amefunguka kuwa hatua ya kutoa wimbo ukiwa kwenye staili ya kuimba imekuja kufuatia maombi kibao aliyoyapata kutoka kwa fans wake.

Akizungumza na Teentz.com muda mfupi uliopita Godzilla anayesumbia kitaa na ngoma kali inayobeba jina la ‘La Kuchumpa’ amesema kuwa ameshangazwa na hataua ya wadau wa muziki wa kizazi kipya kuhoji juu ya uamuzi wake wa kutumia staili ya kuimba kwenye wimbo wake mpya uliopewa jina la ‘nataka’.
“Unajua mimi ni mwanamuziki na katika hilo ni lazima ujuwe kuwa nina mashabiki ambao kwa lolote wako nyuma yangu , hivyo basi walinifuata na kuniambia kuwa wanataka nijaribu kutoa wimbo kwenye staili ya kuimba soo kwakuwa ninatambua umuhimu wao nikaamua kutoa nyimbo mbili moja ikiwa kwenye mtindo huo na nyingine ikiwa kwenye hip hop kama kawaida” alisema Zilla na kuongeza kuwa nimeamu a kufanya hivyo ili kuwarizisha mashabiki wangu wote.