RAY C AFUNGUKA JUU YA NDOA YAKE


MSANII Rehema Chalamila ‘Ray C’ au unaweza kumuita ‘kiuno bila mfupa’ utakuwa haujakosea, amefunguka na kudai kuwa mikakati yake ya ndoa na bwana ake wa Kenya bado inaendelea lakini wanaochelewesha ni wazazi wa mwanaume ambao wanaonekana kuchukua muda katika kutoa maamuzi.Kufunguka kwa msanii huyo kumekuja siku chache baada ya kuzungumza na mwandishi wetu, ambapo alidai kuwa hataki kufanya mambo haraka haraka kwani muda bado upo wa kutosha.

Ray C stejini


Msanii huyo alipoulizwa kuwa tangu iliposikika anataka kuolewa huko nchini Kenya ni muda mrefu umepita ni kitu gani kinachokwamisha, alijibu kuwa kwa upande wake yupo tayari lakini upande wa mwanaume ndiyo wanaochukua muda kutoa maamuzi lakini anaamini kuwa kila kitu kitaenda kama walivyopanga.


“Kila kitu kinakuwa na mipango hivyo sitaki kufanya mambo haraka halafu mwisho wa siku watu waje kunicheka, eti ndoa yangu imevujika sitakimie,”
aliongeza.