SHILOLE ANUSURIKA KUVULIWA NGUO BARABARANI


Zuwena Mohamed ‘Shilole’.
MSANII wa filamu na muziki wa Pwani, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameponea chupuchupu kuvuliwa nguo barabarani maeneo ya Darajani mjini hapa baada ya kukatiza mitaa ya sokoni akiwa katupia kigauni kifupi ajabu. Bongowood ilimshuhudia Shilole akiwa na wanenguaji wake akipigiwa kelele na wanaume waliotaka kumkamata wamvue kisha wamlambe viboko hivyo akalazimika kukimbilia dukani akanunua dela na kulivaa juu ya kigauni cha kihasara alichokuwa amekitinga.