NISHA ALINADI PENZI LAKE JIPYA


SIKU chache baada ya kutangazwa kuwa amemwagana na mpenzi wake Godfrey,  mcheza sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ameibuka na kujinadi kuwa amepata kifaa kipya.

Kupitia akaunti yake ya Facebook, Nisha alibainisha kuwa tayari yupo ndani ya himaya mpya ya mapenzi ingawa pia bado hawezi kuiweka hadharani kwa sababu ya mwezi mtukufu wa Ramadhan.

“Love him to death…Oh God im in loooove. Ah baada ya muda mrefu kuumia..”
ameandika Nisha mtandaoni na kupongezwa na wadau wake.