"UNAYAJUA YALIYOMKUTA AMINA CHIFUPA?.....SASA TUKUONE UMEKUWA MWANASIASA".......HIVI NI VITISHO KWA LOVENESS WA CLOUDS FM


Unakumbuka kuna muda mtangazaji wa Clouds FM Loveness aka Diva alitangaza kuwa mwaka 2015 atagombea ubunge? 
Well, hakuwa anatania kwani hivi karibuni alianza kwa kuchukua kadi ya uanachama wa CHADEMA......
Diva akionesha kadi yake ya uanachama wa CHADEMA

Lakini pamoja na kuchukua uamuzi huo, jana Diva amesema amepewa vitisho kutoka baadhi ya watu kuwa hatofika popote na huenda yakamtokea kama ya marehemu Amina Chifupa.


“Kuna watu walinikalisha chini 4hours, wananiambia umemuona Amina Chifupa, kaishia wapi?! Basi niliogopa sana,” alitweet kumweleza mbunge wa jimbo la Kawe mheshimiwa Halima Mdee.


“Don’t tell me u give in so easily…..I thought i knew you…..kumbe mwoga?umenidisappoint!,” alisema Halima.


Mazungumzo na mheshimiwa Mdee yalimpa nguvu kidogo mtangazaji huyo ambaye aliandika,

 “Really?Basi Umerudisha imani yangu, Its official am in , Joining the movement , sitagive up tena,tatizo my friends hate politics.”