
Mgonjwa  akihamishwa kutoka Wodi ya Kibasila katika Hospitali ya Taifa ya   Muhimbili (MNH), iliyopo Dar es Salaam jana,  ili kupelekwa katika   hospitali nyinyine kutokana na tihsio  la kuwepo kwa mgomo wa madaktari
katika hospitali hiyo na nyingine za serikali sehemu mbali mbali nchini wanaodai stahiki zao mbali mbali, kwa madai ya serikali kushindwa kuzitekeleza
katika hospitali hiyo na nyingine za serikali sehemu mbali mbali nchini wanaodai stahiki zao mbali mbali, kwa madai ya serikali kushindwa kuzitekeleza
MADAKTARI  nchini wameanza mgomo katika baadhi ya hospitali nchini  baada ya  Serikali kushindwa kutekeleza madai yao waliyowasilisha katika  Kamati  ya Majadiliano iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.  Mgomo  huo  umetangazwa na Jumuiya ya Madaktari nchini huku ikifafanua kwamba  kati  ya madai kumi waliyotaka yatekelezwe na Serikali, hakuna hata moja   lililofanyiwa kazi. 
 Hata hivyo,  jana madaktari hao ambao walikaa vikao   vya majadiliano na Serikali kwa siku 90 baada ya kusitisha mgomo wao  wa  pili, wamesema katika madai yao kumi, hakuna hata moja  lililotekelezwa  na Serikali.  Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Dk Stephen  Ulimboka jana  aliwaeleza waandishi wa habari kwamba ili warejee kazini,  Serikali  inatakiwa kutekeleza madai yao yote na kusisitiza kwamba dai  lao la  kwanza ni kuitaka Serikali kuboresha huduma za msingi kwa  wagonjwa.