WAREMBO WA REDD'S MISS HIGHER LEARNING DODOMA 2012 HAWA HAPA

Washiriki wa Redd's Miss Higher Learning Dodoma 2012, wakiwa katika picha ya pamoja katika kambi yao ya mazoezi iliyopo katika Ukumbi wa NK Club mjini Dodoma leo. Warembo hawa watapanda jukwaani Ijumaa hii kuwania taji hilo.
Warembo 11 wa Redd's Miss Higher Learning Dodoma wanataraji kupanda Jukwaani May 18,2012 katika ukumbi wa Kilimani mjini Dodoma kuwania taji hilo kwa mwaka huu.

Show hiyo inataraji kuzindikizwa na Mwimbaji bora wa Kiume wa Tuzo za Kili Music Award 2012, Barnaba kutoka kundi la THT ambaye kwa sasa anawika na wimbo wake wa Magubegube.

Shindano hilo mbali na kudhaminiwa na REDD'S, pia limepata udhamini wa Nokia, Star Time, Nina’s Fashion, Shabby Bus, Clouds FM, African Dream, Club 84, Radio Kifimbo, Salama Salon, Jambo Leo, Mapouder Cosmetics, Emage For You, Salome Boutiq, Dicentman Blog, Joseph Lukaza Blog, na CafĂ© La’Tino.