MAMBO YA BIG BROTHER: HATIMAYE GOLDIE ATIA MGUU NCHINI KENYA NA KUPOKELEWA NA PREZZO


Prezzo & Goldie
Aliyekuwa mmoja wa washiriki na wawakilishi wa Nigeria katika jumba la Big brother Stargame 2012 Goldie, jumamosi iliyopita 15thsept 2012 aliland katika ardhi ya Kibaki mishale ya midnight.
Kwa mujibu wa mtandao mmoja wa Kenya Goldie alipokelewa uwanja wa ndege na yule yule wanaepatana na kukosana mara kwa mara Prezzo, kitu kinachowafanya watu wengi waamini kuwa sasa  uhusiano kati ya Prezzo na Goldie umerejea katika hali nzuri. 
 
pamoja na Prezzo alikuwepo pia former house mate mwingine wa Big Brother aitwae Millicent Mugadi.

Muda mfupi baada ya Goldie kuwasili uwanja wa ndege, mabegi yake yalipelekwa katika Mercedez Benz E-Class rangi ya silver ya Prezzo ambayo ndio iliyompeleka katika hotel aliyofikia.

Ujio wa Goldie nchini Kenya umekuwa wa kimya kimya kitu kinachoashiria kuwa yeye pamoja na mwenyeji wake Prezzo hawakupenda attention ya media.

Kwa mujibu wa watu wa karibu, Goldie amesema atakuwepo Kenya kwa muda wa wiki nzima au na zaidi, na lengo la safari yake hiyo ni kufanya recording ya nyimbo, na kati ya nyimbo atakazo record anategemea kumshrikisha Prezzo.

Ni mwezi mmoja tu umepita toka Prezzo aende nchini Nigeria anakotoka Goldie, kwa lengo la kukutana na Goldie ambaye mara yao ya mwisho kuwa pamoja ilikuwa ni katika jumba la Big Brother ambapo Goldie alikuwa evicted na kumwacha prezzo.