MAPRODUCER WA NIGERIA WAMPA SHAVU "ODAMA" LA KULA BATA UINGEREZA NA MALAYSIA


Staa wa tasnia ya filamu za Kibongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amekula shavu la kufanya ziara ya kikazi nchini Malaysia na Uingereza.
Rafiki wa karibu wa Odama aliiambia Mpekuzi kuwa staa huyo aliondoka nchini hivi karibuni baada ya kupata shavu kutoka kwa maprodyuza wa  Nigeria ambapo atafanya nao ziara ya kikazi katika nchi hizo mbili kisha atarejea Bongo kuleta maujuzi ya kuendeleza tasnia hiyo.