MISS
Ruvuma 2006/07 , Isabela Mpanda ‘Bella’ amefunguka kuwa mwanaume wake
anapomchezea nywele na maeneo nyeti na kifuani huwa habari yake
inakwisha kabisa na kujikuta hoi bin taabani.
Bella anayewakilisha Kundi la Bongo Fleva la Scorpion Girls ameropoka kuwa anapokuwa kwenye sita kwa sita huwa hana ujanja pale mpenzi wake, mwanamuziki Kalama Masoud ‘Luten’ anapomchezea nywele kichwani na ‘chakula ya mtoto’ kifuani.
“Sijui huwa najisikiaje lakini nashangaa tu mizuka inanipanda, inakuwa… kaazi kwelikweli!,” alifunguka Bella.
Kuhusu kuhusishwa na skendo za kutoka na wanaume tofauti, Bella alichomoa na kudai kuwa kazi yake ya sanaa ndiyo inayomkutanisha na wadau tofauti na si kila mwanaume atakayetajwa then anavunja naye amri ya sita.