HUU NDO MOYO WA "CHUMA" WA JACK PATRICK USIO NA CHEMBE HATA MOJA YA HURUMA

 
 MATENDO anayofanya mwanamitindo Jackline Patrick wakati mumewe Abdullatif Fundikira akiteseka gerezani, yametajwa kuwa ni usaliti wa asilimia miamoja na kwamba kama hatajirekebisha, mwisho wake utakuwa mbaya.

 Hayo yamekuja kufuatia hivi karibuni kupatikana kwa picha zinazomuonesha mwanadada huyo akiwa kimahaba zaidi na modo mwenzake wa kiume, Martin Kadinda  huku mume wake akisota nyuma ya  nondo.

Picha hizo zinawaonesha wawili hao wakiwa wamekumbatiana na kufanyiana mambo yasiyostahili kufanyika mbele za watu pale walipokuwa wakiogelea kwenye moja ya fukwe zilizopo jijini Dar na nyingine wakijiachia klabu.

 
HUYU  NDO  MUME WAKE AKIWA GEREZANI
 

 HUYU  NDO JACK  AMBAYE NI  "MKE WA MTU"  AKILA  BATA NA  MWANAUME MWINGINE AMBAYE NI MARTINE KADINDA