JK: Ampa Pole Katibu Wa Mufti Wa Zanzibar Aliyemwagiwa Tindikali

 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali na kumpa pole Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhili Soraga ambaye amelazwa katika chumba cha dharura katika Hospitali ya Taifa ya Muhiombili kufuatia majeraha ya usoni na kifuani yaliyotokana na  kurushiwa Tindikali na watu wasiojulikana wakati akifanya mazoezi katika Kiwanja cha Mwanakwerekwe mjini Unguja juzi

Rais ambaye amerejea  leo Jumanne Novemba 6, 2012 akitokea katika ziara ya kikazi ya  takriban juma moja katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida, amemtakia Sheikh Soraga nafuu ya haraka.
PICHA NA IKULU