Kukataa Posho Ilikuwa Unafiki


Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia CCM Mhe Peter Serukamba amesema suala la baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupinga posho lilikuwa ni unafiki. Serukamba aliyasema hayo katika kipindi cha Makutano kinachoendeshwa na Fina Mango kupitia Magic FM. Fina aliuliza moja ya swali kutoka kwa wasilizaji ambapo alisema biashara ya kukataa posho ni unafiki tu huku akimwambia Fina ataje mbunge gani karudisha au kukataa posho, alisema "Tumeongezewa mafuta tumechukua, tumeongezewa vingine tumechukua hakuna ambaye amerudisha na next day ilipokuwa confirmed wengine wakaanza kukopa" huku akisema hakuna umuhimu wa kupinga posho za wabunge badala yake wabunge waombe serikali iwaongezee posho na watumishi wengine. Alipoulizwa kwa nini wasiiombe serikali ianze na sehemu nyingine kabla ya kuwaongezea mshahara wabunge akitolea mfano wa shiri