KCB Bank Yatoa Msaada Hospitali Za Amana Na Mwananyamala

 Mkuu wa Kitengo Mauzo na Huduma kwa wateja na Jamii  wa benki ya KCB Christina Manyeye akimkabidhi Mganga msaidizi wa Hospitali ya Amana  DK.Shaany Mwaruka  msaada wa Kitanda cha kusaidia wajawazito kujifunguria (Delivery beds)  wkati wa hafla iliyofanyika katika Hospitali hiyo jijini Dar es Salaam.Jumla ya Vitanda Vitano  na Mashine moja ya kutunzia watoto  ambao wanezaliwa  kabla ya muda wake vyote vikiwa na Thamani ya shilingi milioni 15,5. Vilitolewa na benki ya KCB.Kushoto ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala Asha Mahita, kulia ni Diwani wa kata ya Ilala Edson Fungo na Matroni wa Hospitali ya Amana Sr.Agnes Mwega.
 Mkuu wa Idaraya ya Uhazini wa beki ya KCB Tanzania Sam Kimath akimkabidhi msaada wa Mashuka 116  Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala Asha Mahita, na Diwani wa kata ya Ilala Edson Fungo wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es salaam, jumla ya vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi Milioni 15,640,000. Vilitolewa msaada na benki hiyo kwa ajiri ya kusaidia hospitali hiyo ya Amana. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo Mauzo na Huduma kwa wateja na Jamii  wa benki ya KCB Christina Manyeye.
 Mkuu wa Kitengo Mauzo na Huduma kwa wateja na Jamii  wa benki ya KCB Christina Manyeye, akimkakabidhi  Mganga msaidizi wa Hospitali ya Mwananyamala DR.chrispian Kayola  Mashine ya Kutunzia joto ya watoto wanaozaliwa kabla ya muda,(babyWarrmer Machine) yenye thamani ya shilingi Milioni 7.8.iliyotolewa na Benki ya KCB Kwa ajili ya kusaidia jamii inayopata huduma katika hospitali hiyo.wanao shuhudia ni Diwani wa kata ya Ilala Edson Fungo na Mganga msaidizi wa Hospitali ya Amana DR.Shaany Mwaruka. Hafla hiyo ilifanyika katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo Mauzo na Huduma kwa wateja na Jamii  wa benki ya KCB  Tanzania ,Christina Manyeye, akiwa amemshika mmoja wa watoto wenye umri wa siku moja waliozaliwa katika wodi ya wazazi ya Amana jijini Dar es Salaam, wakati alipotembelea waodi hiyo, baada ya kutoa msaada wa Mashuka 116 na Mashine ya joto ya kutunzia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati wake  ( Baby Warmer Mashine) Vitanda Vitano vya kujifungulia akina mama wajawazito vvyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 15.640.000.Vilivyotolewa na Benki ya KCB Tanzania.


Na Mwandishi Wetu

Benki ya KCB Tanzania, imetoa msaada wa vifaa  kwa wodi ya akina mama wajawazito vyenye thamani ya shilingi milioni 15,640,000 kwa hospitali  ya  Amana katika uzinduzi wake wa   wiki ya jamii
Akizungumza katika hafla fupi ya mabidhiano ya vifaa hivyo hivyo yaliyofanyika hospitalini hapo,  Mkuu wa kitengo cha masoko na jamii wa benki ya KCB Christine Manyenye  alisema  Msaada huo uanalenga kupunguza vifo vya aikina mama na watoto Manyenye  alisema kuwa, Benki ya KCB inatambua umuhimu wa  afya ya mama na motto na ndiyo maana iliona ni jambo zuri kuelekeza msaada huo muhimu kwakundi hilo Kila mwaka huwa tunaadhimisha wiki ya jamii kwa kutoa misaada kwa jamii. Kwa kawaida tunaangalia sehemu yenye kuhitaji sana msaada na kutoa mchango  sehemu hiyo. Kwa mfano tumegundua kuwa hospitali zetu haswa hizi zinazohudumia watu wenye kipato cha chini zina matatizo mengi na ndiyo maana leo tumekuja kutoa mchango hapa Amana,Alisema  "Ni matumaini yetu kuwa, vifaa hivi vilivyotolewa na Benki ya KCB vitachangia kwa kiasi kuboresha utoaji huduma kwa akina mama na watoto na hivyo kujenga taifa lenye afya na nguvu," aliongeza.
Mwakilishi wa mganga mkuu wa hospitali hiyo  Docta Shani Mwaruka aliishukuru Benki ya KCB kwa msaada huo na kusema kuwa utasidia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma kutokana na kupatiwa vifaa Hali za hospitali zetu hizi za serikali siyo nzuri sana kutokana na ukosefu wa vitendea kazi, hakika tuahitaji msaada ili tuweze kutoa huduma bora na ndiyo maana tunatoa shukrani za pekee kwa benki ya KCB," alisema Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na mashine ya joto kwa watoto wachanga waliozaliwa bila kutimia 1, vitanga vya kujifungulia 5, vifaa vya kusaidia wakati wa akina mama kujifungua 10, mashuka 116, drums 20 na Cord clamp 100

MWANANYAMALA

Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam, jana imepokea msaada wa mashine ya joto kwa watoto waiozaliwa bila kutimia (baby warmer )  yenye thamani ya shilingi 7,850,000 kutoka katika Benki ya KCB Tanzania Akizungumza wakati wa makabidhiano ya msaada huo, mkuu wa kitengo cha masoko wa benki hiyo Christine Manyenye  alisema msaada huo umetolewa baada ya kubaini uwezo mdogo wa hospitali za umma kuhudumia watoto wanaozaliwa bila kutima (pre mature) kutokana njha ukosefu wa vifaa , Kabla ya kufukia uamuzi wa kutoa msaada huu tulichunguza na kugundua kuwa huduma kwa watoto walizaliwa kabla ya muda wao wa kuzaliwa bado si nzuri kutokana na ukosefu wa vifaa. Tuliona ni jambo zuri kueleza msaada wetu kwa kundi hili" alisema Manyeye alisema kuwa benki ya KCB imekuwa ikielekeza zaidi misaada yake kwenye makundi yenye mahitaji  makubwa na yenye uchache wa rasilimali za kutatua matatizo yake .
Mwakilishi wa mganga mkuu wa hospitali hiyo  Mwananyamala Docta Chrispian Kayolai aliishukuru Benki ya KCB kwa msaada huo na kusema kuwa utasidia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma kwa watoto wanauzaliwa kabla ya muda wao Tunachangamoto nyingi ambazo tunakutana nazo wakati wa kutoa huduma na haswa kwa ajili ya vitendea kazi. Msaaada huu tulioupokea leo utasaidia sana kuboresha huduma na tuna kila sabau ya kuishukuru sana benki ya KCB," alisema Kwa mujibu wa Manyenye, katika kuadhimisha wiki ya jamii hospitali za KCM Moshi, Mwembeladu Zanzibar, Morogoro na Mount Meru ya Arusha itanufaika na misaada itakayogharimu shilingi milioni 79,040,000/-