Zamani ilikuwa ni kawaida kuona wanawake  wanatoboa  masikio, pua, ili kuvaa aina mbalimbali za herini na shemeri. 
 Siku hizi si ajabu kuona wanaume na wanawake wakijitoboa au kuchorwa  alama (tattoo)
 sehemu mbalimbali za miili yao kama kwenye pua,  mdomo, ulimi, tumbo, 
masikio, mikono, miguu, kwenye kichwa, mapaja,  mgongo  na hata sehemu 
za siri yote haya kwa ajili ya urembo, miila au  desturi zao, kutaka 
kujinasibu na tabaka fulani au kutaka kuonyesha  ubunifu wao (artistic expression).
 Kutoboa/kuchorwa mwili kama kutafanywa na  mtaalamu wa kutoboa/kuchora mwili hakuna madhara yoyote ya kiafya. Madhara
 ya kutoboa/kuchorwa mwili  hupatikana pale tu ambapo kitendo  hiki 
 hufanywa na mtu ambaye si mtaalamu na mjuzi wa fani hii bila  kutumia 
njia salama za kiafya.
 Ni mambo gani ya kuzingatia kabla ya kutoboa/kuchorwa  mwili wako?
 1.Unatakiwa kujua  uwezekano wako wa kupata  maambukizi
 - Kama tayari una maambukizi au una kidonda kilichowazi, ni  bora 
ukaacha kutoboa/kuchorwa mwili mpaka utakapopona na kuwa na afya  
njema. 
Hatari ya kupata maambukizi ni kubwa kama utatobolewa/kuchorwa na  mtu ambaye si mtaalamu na hana ujuzi wa kufanya kazi hii.
 Hakikisha
  anayekufanyia  hivi awe anafahamu masuala ya kukinga wateja wake na  
maambukizi ambayo ni pamoja na kusafisha vifaa vyake kila baada ya kazi,
  kuvichemsha vifaa hivyo au kuhakikisha vipo salama na havina bakteria 
 wowote kwa kutumia kemikali za kusafishia, kuvifunika vifaa hivyo baada
  ya kuvisafisha na yeye mwenyewe kuvaa gloves salama (surgical gloves) wakati  wa kufanya kazi yake hiyo ili hata kama ana magonjwa ya kuambukiza  asiweze kukuambukiza wewe kwani 
 2.Hakikisha huna maradhi yoyote sugu
 - Kama  una maradhi ya kisukari, ni bora ukaepuka kutoboa/kuchorwa 
mwili kwani  kidonda chake kinaweza kisipone haraka na hatari ya 
maambukizi kwa  wagonjwa wa sukari iko juu kupitia kwenye vidonda.
 3.Fahamu kuhusu uwezo wako wa kupona - Unatakiwa uwe na ufahamu juu ya uwezo wa mwili wako katika kupona (healing tendencies)  kidonda chochote kile. 
Kuna
 watu wengine wanapopata mchubuko au  kukatika ngozi zao hupona kwa 
ngozi ile kufanya kama baka na uvimbe  unaojulikana kama keloids. 
Kama wewe ni mmoja wa watu wa aina hii basi  unahitaji kuepuka kufanya kitendo hiki cha kutoboa/kuchora mwili wako. 
 Sehemu
 ambazo huchukua muda mrefu kupona baada ya kutoboa/kuchora mwili  ni 
pamoja na kwenye maeneo ya tumboni, kwenye chuchu na hata sehemu za  
siri kwa wanawake.
 4.Jua maumbile yako-Sio
 kila ngozi ya  mwanadamu inafaa kwenye kuitoboa/kuchora, mfano, wale 
wenye ngozi  ya  kwenye tumbo iliyoenuka ndio hufaa kutoboa sehemu hii, 
kama unataka  kutoga ulimi na ulimi huo ni mfupi kutokana na umbile 
lako, (Tongue with short frenum) yaani wale wenye mkunjo chini ya ndimi zao  na hivyo kufanya ulimi kuwa mfupi, hawapaswi kutoga ndimi zao.
 5.Hakikisha unafanyiwa na mtaalamu wa fani  hii.Wataalamu
 wa mambo ya kutoboa/kuchora mwili wana uelewa mkubwa wa  maumbile ya 
mwanadamu na huwa na vifaa vya kuzuia uvujaji wa damu pindi  unapotokea.
 Pia huwa na ufahamu wa jinsi ya kukulinda na maambukizi .
 6.Historia yako ya afya-
 Wataalamu wa  kutoboa/kuchora mwili wanatakiwa kuchukua historia ya 
 afya ya wateja  wao inayohusisha magonjwa ya moyo, ugonjwa wa kisukari,
 mzio/aleji,  ugonjwa wa pumu na kadhalika.
 Kama
 unatumia dawa za ugonjwa wowote ule  ni bora ukamweleza mapema mtaalamu
 huyo kabla hajaanza  kukutoboa/kukuchora mwili wako.
 Ili kuzuia uvujaji wa damu kwa wingi,  unashauriwa kuepuka dawa aina ya aspirin angalau kwa wiki moja kabla ya kutoboa/kuchora mwili  wako, pia epuka dawa jamii ya Non Steroidal Anti-Inflammataory Drugs (NSAIDS) kama ibuprofen, naproxen na kadhalika.
 7.Hakikisha vifaa sahihi ndivyo  vilivyotumiwa-
 Hakikisha ya kwamba  vifaa vinavyotumiwa ni vile ambavyo  havina   
madini ya Nickel, pini zenye ubora na vipachiko vya aina  mbalimbali 
ambavyo ni vya ubora wa hali ya juu. 
Pini na vipachiko vidogo  vinaweza kutoka na kusogea kutoka katika sehemu vilipopachikwa na hivyo  kukuletea madhara makubwa.
 8.Mfumo wa maisha-
 Kipachiko cha katika  maeneo ya tumboni (kitovuni, chini ya kitovu nk) 
huvutia kwa mwanamke  wenye umri mdogo wa miaka ya ishirini na huleta 
picha mbaya kwa wanawake  wale waliofikia umri wa miaka thelathini na 
kuendela.
 Unatakiwa
  uangalie  na aina ya taaluma yako  kama inaendana na vitu vya aina 
hivi,  mathalani wewe ni mwanamume unafanya kazi ya mhudumu wa afya, 
mwalimu,  askari,  unafanya kazi kwenye ofisi, muuzaji bidhaa kwa 
wateja, mtoa  huduma za kijamii, halafu unavaa herini kwenye masikio, 
ha! Watu  watakuchukuliaje?
Hakuna
 atakaye kuelewa au kukubali kuhudumiwa na wewe.  Pia angalia kama 
 mila, desturi, dini  yako kama inakubali mambo haya  kwani itakuwa 
jambo la aibu sana kama utatoga mwili wako  bila  kuzingatia mazingira 
unayoishi kwani binadamu tunaishi kulingana na  mazingira yetu. 
Hii
 sio kwa wanaume tu hata kwa wanawake, kabla ya  kutoboa/kuchora  sehemu
 husika zingatia  taaluma yako, mila,  desturi,mazingira,  dini yako nk.
 9.Fuata maelekezo vizuri-
 Fuata maelekezo  unayopewa vizuri jinsi ya kujikinga na maambukizi 
baada ya  kutoboa/kuchorwa mwili wako, namna ya kusafisha sehemu husika 
nk.
 10.Fahamu madhara ya kutoboa/kuchorwa sehemu  husika-
 Fahamu kuhusu madhara ya kutoboa/kuchorwa sehemu husika kwanza  kabla 
ya kutoboa/kuchorwa ili uweze kujiepusha na madhara hayo.
Pia
  unatakiwa ujue sehemu hiyo unayotoboa/kuchora, kidonda chake kinapona 
 baada ya muda gani na maumivu yake huchukua siku ngapi kuisha? 
Hatma ya  afya yako ipo mikononi mwako!  Tafakari!
