RAMIREZ AITWA TENA BRAZIL.

KIUNGO wa kimataiafa wa Brazil, Ramirez ameitwa tena katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo kinachonolewa na kocha Mano Menezes kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Sweden ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014. Ramires mwenye umi wa miaka 25 amekuwa tegemeo katika klabu yake ya Chelsea ambayo aliiwezesha kushinda taji la FA pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita lakini hakujumuishwa katika kikosi cha Brazil toka alipoitwa katika michuano ya Copa Amerika 2011. Lakini Menezes ameamua kumjumuisha kiungo huyo ambayo atacheza pamoja na wachezaji wenzake ambao wanacheza klabu moja David Luis na Oscar. Katika kikosi hicho kocha huyo amewaita wachezaji walewale waliopo katika kikosi cha Olimpiki na kuongeza wengine kidogo ambao wataziba nafasi za wale ambao watapumzika baada ya olimpiki. Mchezo wa kirafiki hidi ya Sweden unatarajiwa kuchezwa Agosti 15 mwaka huu.