CECAFA YASIFU NIDHAMU KATIKA MICHUANO YA KAGAME.
  | 
|   | 
Baraza la vyama vya soka 
Afrika mashariki na kati CECAFA limevipongeza vilabu vyote vilivyo 
fanikiwa kufikia katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Kagame 
ambayo inaendelea nchini Tanzania. Jumla
 ya timu nane zimefanikiwa kuingia katika hatua hiyo wakiwemo mabingwa 
watetezi wa kombe Yanga ambao waliongoza katika kundi B kwa kumaliza 
hatua ya makundi wakiwa wamejikusanyia jumla ya points 6 kufuatia kupata
 ushindi katika michezo miwili dhidi ya Salaam Wau ya Sudani kusini na 
ARP ya Rwanda na kupoteza mchezo mmoja dhidi ya Atletico ya Burundi. Timu nyingine ni Simba, URA na Vita Club toka kundi A na Azam na Mafunzo toka kundi C. Katika kundi la B yanga imeungana na APR na Atletico kucheza hatua ya mtoano. Akizungumza
 hii leo katibu wa CECAFA Nikolaus musonye amesema wao kama CECAFA 
wameridhishwa na viwango na nidhamu iliyoonyeshwa na timu zote huku 
akisifu zaidi mchezo wa jana kati ya Simba na Vita ambao ulimalizika kwa
 nidhamu ya hali ya juu pasi na kuwepo kadi hata moja ya njano wala 
nyekundu. Katika 
hatua nyingine CECAFA imefanya marekebisho ya siku katika ratiba ya 
michuano hiyo kuanzia hatua ya nusu fainali kwa kutenganisha michezo ya 
hatua hiyo endapo timu mbili kubwa za Tanzania Simba na Yanga endapo 
zitafanikiwa kuingia katika hatua ya nusu fainali. Musonye
 amesema endapo timu hizo mbili za Tanzania zenye mashabiki wengi 
zitafuzu hatua hiyo basi mchezo wa nusu fainali ya kwanza itachezwa 
jumatano na mchezo wa pili utachezwa alhamisi tofauti na ilivyo sasa 
ambapo michezo ya nusu fainali yote inaonekana kwenye ratiba kuchezwa 
siku moja yaani alhamisi. Amesema hili limezingatia hali ya usalama endapo timu moja itaonekana kupoteza mchezo wake. Timu ambazo zimeaga michuano ni Ports ya Djibout, Salaam Wau ya Sudan Kusini na Tusker ya Kenya.