"NILIANZA KUSIKIA KIZUNGUZUNGU NA KUONA GIZA NENE KABLA YA GARI YANGU KUPINDUKA"....NISHA


NISHA ambaye ni msanii wa filamu  hapa nchini ameamua kuvunja ukimya   na  kusimulia kinagaubaga juu ya ajali iliyomtokea majuzi wakati akitoka location na kusema kuwa kabla ya kupata ajali alikua mzima kabisa na aliweza kufanya kazi zake zote locationa mpaka mida ya saa saba za usiku...
"Wakati anarudi nyumbani anasema alifika sehemu akajisikia kizunguzungu na kuona kiza baada ya hapo ndipo aliposhtukia akiingia porina na gari kupinduka na kupata ajali hiyo".....NISHA

Nsha anadai kuwa  hataki kulihusisha tukio hilo na kitu chochote bali ni mipango ya mwenyezi mungu na amesema kwa sasa hali yake si nzuri sana hivyo anaomba watanzania wamuombee ili aweze kupona haraka na aweze kurejea katika shughuli zake kama kawaida


DIAMOND NAYE ANUSURIKA  KUFA.....

Juzi Diamond akiwa na gari lake alipata ajali ambayo ilisababisha sehemu ya mbele kuharibika. Kwa mujibu wa meneja wake, Raqey Mohamed wa I-View Media ajali hiyo ilisababishwa na mwendesha pikipiki..